URUSI NA URENO VITANI LEO KOMBE LA MABARA


Michuano ya kombe la mabara itaendelea tena leo hii kwa michezo miwili ya kundi A kuchezwa, wenyeji Urusi watashuka katika dimba la Otkrytiye Mjini Moscow, kucheza na Ureno .
 CONF

Mwamuzi Gianluca Rocchi kutoka Italia ndie atakae chezesha mchezo huo wa wenyeji na Ureno na mchezo huo utacheza saa kumi na mbili jioni kwa saa za Afrika mashariki.

Na mchezo wa pili wawakilishi wa bara la Afrika katika michuano hiyo timu ya Cameroon watashuka katika dimba la Fisht Olympic kupepetana na New Zealand , mchezo huo utachezeshwa na mwamuzi Bakary Gassama kutoka Gambia.
Urusi ndio vinara wa kundi A wakiwa na alama tatu baada ya kupata ushindi dhidi ya New Zealand, Ureno na Cameroon wao wana alama moja moja na New Zealand wanaburuza mkia wakiwa hawana alama hata moja.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment