Michuano ya kombe
la mabara itaendelea tena leo hii kwa michezo miwili ya kundi A
kuchezwa, wenyeji Urusi watashuka katika dimba la Otkrytiye Mjini
Moscow, kucheza na Ureno .
Mwamuzi Gianluca Rocchi kutoka Italia
ndie atakae chezesha mchezo huo wa wenyeji na Ureno na mchezo huo
utacheza saa kumi na mbili jioni kwa saa za Afrika mashariki.
Na
mchezo wa pili wawakilishi wa bara la Afrika katika michuano hiyo timu
ya Cameroon watashuka katika dimba la Fisht Olympic kupepetana na New
Zealand , mchezo huo utachezeshwa na mwamuzi Bakary Gassama kutoka
Gambia. Urusi ndio vinara wa kundi A wakiwa na alama tatu
baada ya kupata ushindi dhidi ya New Zealand, Ureno na Cameroon wao wana
alama moja moja na New Zealand wanaburuza mkia wakiwa hawana alama
hata moja.
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
0 comments :
Post a Comment