HAIJULIKANI Mapango ya Amboni yaligunduliwa lini,taarifa zilizopo ni kwamba watu wa makabila yaliyoishi jirani na eneo hilo, Wadigo,Wasambaa,Wabondei na Wasegeju,walikuwa wakiyatumia kwa ajili ya matambiko ya mizimu tangu Karne ya 16.
Eneo la Mapango hayo wakati huo lilijulikana kwa jina la Mzimu wa Mabavu,Watu kutoka sehemu mbalimbali ndani na nje ya nchi,hufika mapangoni hapo kwa ajili ya kuomba au kutambika.
Kampuni ya Amboni Limited,iliyokuwa ikimiliki mashamba ya Mkonge katika mkoa wa Tanga,ilimiliki eneo hilo la mapango mwaka 1892,ili kulitumia kama sehemu ya kupumzikia.
Serikali ya Tanzania ilianza kutangaza eneo la mapango hayo kuwa eneo la hifadhi mwaka 1922,baada kujlishwa mapango hayo na wamiliki wa Amboni Limited.
Mwaka 1937 Serikali ilipitisha Sheria ya mambo ya kale (Monuments preservation ordinance of 1937) iliyofuatiwa na ile ya mwaka 1953 ambayo imesaidia kulinda mambo ya kale.
Mapango hayo yalitokana na mabadiliko ya nguvu za asili,zilizobadilisha maumbile ya miamba ya chokaa kipindi cha Jurasiki (Jurassic period) miaka milioni 150 iliyopita.
Kulingana na utafiti uliofanywa, eneo hilo la Mapango,lilikuwa chini ya maji miaka milioni 20 iliyota, na linakadiriwa kuwa na ukubwa wa kilomita za mraba 234,lenye mazingira ya uoto wa asili.
NJIA ZILIZOSABABISHA MAPANGO
Utafiti uliofanywa Mturi (1975) njia ya kwanza ni ya maji ya Mvua yanapochanganyika na hewa ya “Carbondioxide” katika anga na kutengeneza tindikali ya kaboni (Carbonic acid) ambayo inauwezo wa kuyeyusha madini ya Calcium Carbonate yanayounda sehemu kubwa ya miamba ya chokaa.
Maji hayo yenye tindikali husababisha mabadiliko yanapoteremka kuelekea aridhini,yafikapo aridhini meza ya maji (Water Table) na yakiendelea kuongezeka,maji hayo yenye tindikali huwa na uwezo wa kuyeyusha maungio ya miamba,na sehemu laini zaidi za miamba na kusababisha nyufa.
Nyufa hizo huzidi kupanuliwa na maji yanayotembea na kusababisha baadhi ya mawe kuporomoka na kufanya mapango.
Kasi ya maji inapozidi njia ndogondogo hupanuliwa na kuwa kubwa zaidi,na inawezekana mapango madogo madogo kuunganishwa na hatimaye kuwa na mfululizo wa mapango kama yanavyoonekana.
- MLANGO wa kuingilia katika Mapango ya Amboni,Mlango huo wenye umbo la Bara la Afrika,ni moja ya vivutio vya Mapango hayo.
0 comments :
Post a Comment