HIFADHI YA SERENGETI

Hifadhi ya taifa ya Serengeti, yenye ukubwa wa kilometa za mraba 14,763, ni hifadhi ya pili kwa ukubwa nchini ( baada ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha).
Serengeti ni moja kati ya hifadhi maarufu sana duniani. Umaarufu wa hifadhi hii unatokana na misafara mirefu ya nyumbu wanao hama kwa makundi makubwa kutoka upande mmoja wa mbuga hadi mwingine, na kuvuka mpaka wa Tanzania hadi hifadhi ya taifa ya maasai mara nchini Kenya. Wakichagizwa na mvua kila mwaka zaidi ya nyumbu milioni moja, pundamilia 200,000, swala 300,000 huunga misafara ya kutafuta malisho na maji. Uhamaji huu umeipataia sifa ya kuwa moja ya maajabu saba ya asili ya Afrika.
Hifadhi ya Serengeti pia ni maarufuu kwa wanyama walao nyama kama chui na simba. Ukubwa wa hifadhi hii umesaidia sana kudumisha uhai wa wanyama walio katika hatari ya kutoweka kama faru weusi na duma. Uwapo Serengeti utashuhudia wawindaji kama duma wanavyowinda, aidha zipo aina mbalimbali zaidi ya 500 za ndege.
Leo kwa ufupi, tutakupatia mambo kumi (10) kuhusu Hifadhi ya Serengeti ambayo ungependa kuyajua na kusimilua kwa wenzanko ambao hawakupata kuyajua;

1.      Mfumo wa Mazingira wa hifadhi ya taifa Serengeti ni kongwe katika dunia. Hifadhi hii inatunza viumbe hai mbalimbali ikiwemo mimea na wanyama ambavyo vingine havipatikani mahali popote duniani.
Mfumi wa uhamaji wa Nyumbu wa Serengeti

2.      Serengeti ni nyumba ya moja ya maajabu ya asili saba ya dunia. Zaidi ya nyumbu milioni moja uhama kwa kuvuka mto Mara na kuelekea hifadhi ya taifa ya Maasai Mara kwa upande wa Kenya katika kutafuta malisho yao. Na hukaa Kenya kwa mwezi mmoja tu na miezi iliyobaki hutumia mda wao wakiwa Tanzania 


Misururu ya nyumbu wakihama kutoka upande mmoja kwenda mwingine katika hifadhi ya Serengeti

3.   Katika miaka zaidi ya milioni moja iliyopita, hifadhi ya Serengeti imebaki kuwa ya asili kwa kiasi kikubwa bila kuathiriwa na mabadiliko ya kimazingira. Wanyama pori, mimea na mikondo ya maji bado kwa kiasi kikubwa ni ya asili kama ilikuwa miaka milioni moja iliyopita. Kwa kushangaza, mabaki ya zamani ya mtu (miaka milioni 2 iliyopita) yaligunduliwa hapa na mtu maarufu Afrika Mashariki archaeologist, Dr. Leakey.


Binadamu wa kale aliepata kuishi maeneo ya serengeti miaka milion 2 iliyopita

4. Watalii wengi huvutiwa na Hifadhi hii na kushuhudia zaidi ya nyumbu milioni moja wakiwa wanahama kwa kufatilia malisho yao. Hata hivyo, punda milia pia huhama pamoja na nyumbu, angalau kwa idadi ndogo.


Pundamila pia huama pamoja na nyumbu katika hifadhi ya Serengeti

5.  Maelfu ya wanyama wanaohama wengine hushindwa kukamilisha safari yao kutokana na kuliwa na mamba na wanyama wengine walao nyama. 


Nyumbu wakivuka moja ya  mito inayopatikana Serengeti
6.    Serengeti National Park inapatika kati ya futi 3020 na futi 6,070 juu ya usawa wa bahari. Hali ya hewa yake kwa ujumla ni kavu lakini inapata mvua nyingi katika miezi ya Juni na Julai


Kipindi cha mvua Serengeti

7.      Serengeti kwa kiasi kikubwa ni ya uoto wa savannah na vichaka vilivyotawanyika na ambavyo ni bora kwa ajili ya wanyama walao nyasi na nzuri kwa ajili ya wanyama walao nyama pia. Miongoni mwa wanyama wapatikanao hapa ni pamoja na, pundamilia, tembo, twiga, nyumbu, swala , paa na nyati. Miongoni mwa wanyama walao nyama wanaopatikana ni pamoja na simba, duma , chui, fisi , mbweha, nk



8.      Serengeti ni chimbuko la jamii maarufu ya Wamasai kabla ya kuhamishiwa katika maeneo ya mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro mnamo mwaka 1959. Wamasai ni moja ya jumuiya za Kiafrika kwamba ambazo bado huishi kwa kuzingatia mila zao za kale na utamaduni kama vile tohara , ngoma na kafara.


Wamasai wakiwinda na silaha za jadi

9.      Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro awali lilikuwa sehemu ya hifadhi ya serengeti mpaka 1951 wakati Uingereza walipolitenga kwa ajili ya utafiti kama binadamu na wanyamapori wanaweza kuishi pamoja katika sehemu moja bila ya kuathirana.



10.      Kwa mara ya kwanza utafiti wa kina juu ya mazingira ya Serengeti ulifanywa na raia wawili wa Ujerumani ( baba na mwana ) , Dk Bernhard na Michael Grizmek . Maelezo ya matokeo ya tafiti za Serengeti ziliwekwa na kuhifadhiwa kama kumbukumbu katika kitabu chao maarufu kinachoitwa “Serengeti shall never die.”  
Dr. Bernard Grizmek na mwanae Michael Grizmek wakiwa katika tafiti zao kwenye Hifadhi ya Serengeti.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment