SPORTPESA YAINGILIA KUOKOA JAHAZI YANGA

Kampuni tajiri ya SportPesa ambao ni wadhamini wapya wa Yanga, imeingilia kati hali kiuchumi ndani ya klabu hiyo na kuokoa jahazi.
YANGA bado ina hali ngumu kifedha. Ni ukweli ingawa hauwaingii akili kirahisi mashabiki wa timu hiyo ambao wameanza kushtuka hasa baada ya mastaa kadhaa kutua Jangwani wakapiga picha na viongozi lakini wakaenda kusaini kwenye klabu pinzani za Simba na Azam.

Image result for picha za klabu ya yanga
 

Kampuni tajiri ya SportPesa ambao ni wadhamini wapya wa Yanga, imeingilia kati hali kiuchumi ndani ya klabu hiyo na kuokoa jahazi.
 
Viongozi wameingia makubaliano maalum na wadhamini hao wakakopeshwa fungu ambalo limetumika kulipa malimbikizo yote ya mishahara na kila mchezaji na mfanyakazi wa Yanga sasa roho kwatu.
 
Sportpesa wamekubaliana kwa siri na vigogo wa Yanga kwamba kwenye fungu hilo walilokopeshwa la Sh400 milioni watakatana juu kwa juu ili mradi mambo yaende sawa na vijana warudi kwenye morali yao na sasa wanajipanga kupata vyanzo vingine tayari kwa usajili mpya ambao Simba wanaufanya kwa fujo kweli kweli.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment