Kampuni tajiri ya SportPesa ambao ni wadhamini wapya wa Yanga, imeingilia kati hali kiuchumi ndani ya klabu hiyo na kuokoa jahazi.
Kampuni tajiri ya SportPesa ambao ni wadhamini wapya wa Yanga, imeingilia kati hali kiuchumi ndani ya klabu hiyo na kuokoa jahazi.
Viongozi wameingia makubaliano maalum na wadhamini hao wakakopeshwa fungu ambalo limetumika kulipa malimbikizo yote ya mishahara na kila mchezaji na mfanyakazi wa Yanga sasa roho kwatu.
Sportpesa wamekubaliana kwa siri na vigogo wa Yanga kwamba kwenye fungu hilo walilokopeshwa la Sh400 milioni watakatana juu kwa juu ili mradi mambo yaende sawa na vijana warudi kwenye morali yao na sasa wanajipanga kupata vyanzo vingine tayari kwa usajili mpya ambao Simba wanaufanya kwa fujo kweli kweli.
0 comments :
Post a Comment