MITANDAO YATAKIWA KUDHIBITI MAUDHUI TATA

Mtandao wa kijamii wa Facebook umetoa tamko kwamba unataka kujitenga na mazingira ya uhasama kwa watu wanaoweka maudhui tata ama watu wenye viashiria ama matendo ya kigaidi. Kauli hii imekuja baada ya Waziri mkuu wa Uingereza , Theresa May, kuzitaka kampuni zinazojihusisha na masuala ya teknolojia kuchukua juhudi za makusudi kukabiliana na maudhui yenye mrengo wa kigaidi.
 
Thereza amesema kwamba makampuni makubwa ya kimtandao zisipokuwa makini zitakuwa zinatoa nafasi kwa vikundi vya wanamgambo wenye itikadi kali kuzaliana.
Kufuatia kauli hiyo , Facebook imetamka kwamba kuanzia sasa itakuwa ikiondoa mara moja, maudhui yenye viashiria vya ugaidi.
Mtandao wa Twitter wao wamejinasibu kwamba kazi hiyo yakuondoa ama kufutilia mbali maudhui tatanishi na kamba mwaka wa jana pekee ulifanikiwa kuondoa maudhui ya aina hiyo kutoka katika akaunti elfu nne na kwamba ulijiongeza katika matumizi ya teknolojia .
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment