DI MARIA AINGIA KWENYE KASHFA

PARIS, Ufaransa
WINGA wa zamani wa Manchester United, Angel di Maria, ameingia kwenye kashfa ya ukwepaji kodi na tayari amekubali kulipa kitita cha Pauni milioni 1.76 ili kumaliza kesi hiyo.

Kwa mujibu wa Mamlaka ya Ukusanyaji Kodi Hispania, Muargentina huyo alifanya uhuni huo alipokuwa akiichezea Real Madrid.

Mchezaji huyo wa PSG kwa sasa, alitajwa kutolipa kodi katika mapato yake ya haki za picha akiwa na mabingwa hao wa La Liga.

Inaelezwa kuwa, hakulipa kitita cha Euro milioni 1.3 katika msimu wa 2012-2013.
Kama si kutenda kosa hilo kwa mara ya kwanza, sheria za Hispania zingemtaka Di Maria kutumikia kifungo cha miezi nane gerezani.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment