BUNGE LA UINGEREZA KUFUNGULIWA

Bunge la Uingereza linafunguliwa leo, katika sherehe ambayo Malkia Elizabeth, atasoma sera ambazo serikali ya chama cha Conservative cha Waziri Mkuu Theresa May kinanuia kutekelezwa
Sherehe za leo zinaonekana hazitakuwa kama za kawaida kwa misingi ya maandalizi na pia katika sera.
 Bunge la Uingereza kufunguliwa huku Malkia Elizabeth akihutubia sera za seriali ya Theresa May

Badala ya kusafiri kwa gari maalum linalovutwa na farasi, na kulakiwa na gwaride la jeshi, Malkia Elizabeth leo atawasili katika majengo ya bunge kwa gari dogo.

Kinyume na utamaduni, hapatakuwepo na mavazi maalum kwa mara ya kwanza tangu 1978
Hali hii imesababishwa na uchaguzi ambao umemuacha waziri mkuu kutokuwa na idadi ya kutosha bungeni ili kuidhinisha miswada, na sasa Bi May anajaribu kuunda muungano na vyama vingine vidogo vidogo, mpango ambao umesababisha hotuba hiyo ya Malkia kucheleweshwa.

Matokeo hayo ya uchaguzi pia yanamaanisha Bi May atalazimika kupuuza baadhi ya sera zake ambazo hazikuwa maarufu.

 Theresa May

Bunge la sasa litatawaliwa na mjadala kuhusu Uingereza kujiondoa kutoka kwa muungano wa Ulaya mbali na muda wa bunge hilo kuongezwa.

Serikali ya Bi May inatarajiwa kuwa na wakati mgumu bungeni, kwa kuwa hakuna serikali ambayo imewahi kushughulikia suala hili na Uingereza kujiondoa kutoka kwa muungano wa Ulaya, huku ikiwa haina wabunge wa kutosha bungeni.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment