Wataalam wa maswala ya angani wametangaza ugunduzi wa sayari nyengine kumi angani ambazo huenda zinaweza kusaidia uhai.
Wanasayansi
wa shirika linaloshughulikia maswala ya angani NASA wanasema kuwa data
mpya iliochunguzwa kutoka kwa darubini ya Kepler inaonyesha sayari kumi
zenye miamba ambazo zipo hatua chache kutoka kwa mkusanyiko wa nyota.
Sayari hizo ambazo zinatoshana na dunia, zote zipo nje ya jua katika mkusanyiko huo wa nyota.
Darubini hiyo ya Kepler sasa imegundua jumla ya sayari 50 katika maeneo tofauti yenye uhai angani.
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
0 comments :
Post a Comment