MOGAE: NI MAPEMA KUMKUBALI MRITHI WA MACHAR

Mkuu wa kundi linalofuatilia utekelezwaji wa mkataba wa amani nchini Sudan Kusini amesema kwa sasa hawawezi kumkubali makamu wa rais mpya aliyeapishwa kuchukua pahala pa Dkt Riek Machar.
Festus Mogae, ambaye ni rais wa zamani wa Botswana, ameambia BBC kwamba uchunguzi unafaa kufanywa kubaini iwapo maafisa waliomteua Taban Deng Gai, walikuwa na mamlaka ya kufanya hivyo.Gai


Bw Deng Gai aliteuliwa na kundi ambalo limekuwa likimpinga Dkt Machar katika mrengo wake wa SPLM
Machar, ambaye aliteuliwa makamu wa kwanza wa rais kama sehemu ya mkataba wa amani kati ya upande wake na Rais Salva Kiir, amepinga kufutwa kazi kwake.

Bw Mogae ameshutumu kile alichosema ni uhasama baina ya wanasiasa nchini Sudan Kusini jambo ambalo anasema limesababisha maafa kwa raia.
Amesema hali nchini Sudan Kusini imeendelea kuwa mbaya, na amesisitiza kwamba kikosi cha kulinda amani cha kanda kinafaa kutumwa nchini humo.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment