FIFA YATETEA TEKNOLOJIA YA KUTUMIA PICHA ZA VIDEO

Shirikisho la soka duniani Fifa limetetea mfumo mpya wa teknolojia ya Video uliobuniwa kuwasaidia Marefa kutoa maamuzi sahihi (VAR) kuwa teknolojia hiyo itafaa sana katika mchezo wa mpira wa miguu siku za mbeleni.
 CONF

Lengo shirikisho hilo la soka ni kuona teknolojia hiyo inatumika katika fainali za michuano ya kombe la dunia ya mwaka 2018 ambazo pia zitachezwa Nchini Russia.

Rais wa Fifa Gianni Infantino amesema : "Tumeona namna teknolojia hii ya video inavyoweza kuwasaidia waamuzi kufanya maamuzi sahihi uwanjani.

Katika maelezo ya Fifa katika matukio matano yaliyotokea kwenye michuano ya kombe la mabara yakaamuliwa na teknolojia hiyo imeonyesha manne ni ya kuzidi na moja ni la mchezaji kushika mpira.
Gianni Infantino anataka Majaribio ya VAR yafanikiwe ili teknoloji hiyo ipitishwe kuweza kutumika rasmi katika fainali zijazo za kombe la dunia.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment