Nyota wa muziki wa Pop nchini Marekani Beyonce amejifungua mapacha kulingana na vyombo vya habari nchini Marekani.
Vyombo
vya habari vya Entertainment Weekely, Us Weekly na People Magazine
vimethibitisha habari hizo lakini tarehe ya kuzaliwa na jinsia ya watoto
haijajulikana.
Beyonce ambaye ni mkewe mwanamuziki wa mtindo wa Rap Jay Z
alitangaza kwamba ni mjamzito katika picha ya Istangram mnamo mwezi
Februari ambapo ni picha iliopendwa mno katika historia ya mtandao
huo. Wawili hao tayari wana mwana wa kike, kwa jina Blue Ivy aliye na umri wa miaka mitano.
Hakujakuwa na tangazo rasmi kuhusu kujifungua huko kutoka kwa Beyonce na Jay Z mwenyewe.
Picha
nyengine zilizochapishwa na Beyonce baada ya kutangaza kuwa ni mjamzito
ziliomuonyesha akiogelea chini ya maji, akiwa katika maua huku akiwa
amekaa uchi ndani shada la maua. Katika picha moja mwimbaji huyo wa wimbo 'Lemonade'
alisimama akiwa uchi na kushikilia tumbo lake na mkono mmoja na
mwengine akishikilia titi lake , mbele ya kichwa cha kiongozi wa zamani
wa Msiri.
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
0 comments :
Post a Comment