DIAMOND ATOA SABABU ZA KUTOSHIRIKI BET


WAKATI msanii pekee kutoka Afrika Mashariki, Ray Vanny akitarajia kuhudhuria hafla za utoaji wa tuzo za BET, zinazotolewa Jumapili hii huko Los Angeles, Marekani, Diamond Platnumz amesema sababu za kutoswa kwenye tuzo hizo mwaka huu imetokana na kupunguza kasi ya kutoa kazi.

Akizungumza jana wakati akitambulisha nyimbo zake mbili mpya, I Miss You na Fire, Diamond alisema lengo lake la kupunguza kasi ya kutoa nyimbo lilikuwa ni kutoa nafasi kwa wasanii wengine.

“Mwaka jana sikutoa nyimbo, nilikuwa nifanya kazi ya kuwashika mkono wasanii pamoja na kuacha wenzangu nao wapate nafasi, ndiyo maana leo hii Ray Vanny anatuwakilisha vyema, lakini mwakani nitaingia tena kwenye tuzo hizo sababu nimeanza kuachia kazi,” alisema Diamond Platnumz.

Mwaka uliopita Diamond Platnumz aliingia kwenye kipengele cha Msanii Bora wa Kimataifa Afrika, ambapo alikutana na wasanii kam Black Coffee, Wizkid, AKA na Tiwa Savage.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment